LITANIA YA FIKRA TAKATIFU SANA YA BWANA WETU YESU KRISTO
Bwana, utuhurumie. Kristo, utuhurumie. Bwana, utuhurumie.
Kristo, utusikie. Kristo, utusikilize.
Baba wa mbinguni, Mungu, uliyetuumba katika Fikra zako, utuhurumie.
Mwana, Mkombozi wa ulimwengu, Mungu, usiyeidharau akili ya mwanadamu,
utuhurumie.
Roho Mtakatifu, Mungu, unayeifikia akili ya mwanadamu kwa ragba takatifu, utuhurumie.
Utatu Mtakatifu, Mungu Mmoja, unayeyaalika makabila na mataifa yote yapate kuishiriki
Fikra yako, utuhurumie.
Fikra ya Kristo, iliyoungana na Fikra ya Baba wa milele,
– utubadilishe.
Fikra ya Kristo, iinayoongoza kwaya za Malaika,
Fikra ya Kristo, inayoundwa katika sala kadiri ya Mapenzi ya Baba wa mbinguni,
Fikra ya Kristo, iliyokabidhiwa kwa malezi ya Yosefu na Maria,
Fikra ya Kristo, inaoykua katika hekima na neema,
Fikra ya Kristo, inayowavutia wasomi na wasio na elimu,
Fikra ya Kristo, iliyowekwa chini ya dhima ya wazi ya wito wake,
Fikra ya Kristo, inayotathmini matukio ya maisha kwa misingi ya maadili ya Kimungu,
Fikra ya Kristo, isiyofanya mapatano na majaribu ya Yule Mwovu,
Fikra ya Kristo, isiyovumilia uovu mahali popote na wakati wowote,
Fikra ya Kristo, inayofunua kila aina ya unafiki,
Fikra ya Kristo, inayojiepusha na kujifanya kwa namna yoyote,
Fikra ya Kristo, isiyotiwa doa na hila ya aina yoyote,
Fikra ya Kristo, iliyojawa amani ya dhamiri safi,
Fikra ya Kristo, iliyo katika umoja wa utashi na hisia,
Fikra ya Kristo, iliyo wazi kwa ukweli kamili,
Fikra ya Kristo, isiyozidiwa na mahangaiko ya maisha ya kila siku,
Fikra ya Kristo, inayolinda daima thamani ya uhai wa binadamu,
Fikra ya Kristo, inayokumbusha hadhi ya asili ya mwanamume na mwanamke,
Fikra ya Kristo, inayochochea maswali juu ya maana ya kina kabisa ya maisha ya duniani,
Fikra ya Kristo, inayothamini nia njema, maneno na matendo mema,
Fikra ya Kristo, inayowakumbuka ndugu na marafiki zetu,
Fikra ya Kristo, inayowatafutia wagonjwa na fukara msaada wanaoustahili,
Fikra ya Kristo, isiyotafuta fursa ya pongezi,
Fikra ya Kristo, isiyokuwa na shauku ya kulipiza kisasi kwa maadui,
Fikra ya Kristo, inayozingatia vigezo sahihi vya kuwasamehe wakosefu,
Fikra ya Kristo, inayowaahidi watubuo neema ya huruma na maisha mapya,
Fikra ya Kristo, inayowaonesha watu mandhari ya heri ya milele,
Mwana-Kondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za ulimwengu,
— utusamehe, ee Bwana.
Mwana-Kondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za ulimwengu,
— utusikilize, ee Bwana.
Mwana-Kondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za ulimwengu,
— utuhurumie.
Kuhani: Ee Mungu, Uliye Ukweli safi na wa pekee.
Waamini: Uzifanye fikra zetu zifafane na Fikra ya Mwanao Mpendwa.
Kuhani: Tuombe. Ee Mungu Mwenyezi na wa milele, Mungu Mmoja katika Utatu
Mtakatifu, ulimuumba mwanadamu kwa sura na mfano wako. Tunakuomba utujalie kwa
nguvu ya Roho Mtakatifu, ili kwa fikra zetu tupate kumtukuza Mwanao sifa anayostahili.
Anayeishi na kutawala nawe daima na milele.
Waamini:
Amina.
tafs. ks. Wojciech Kościelniak, mishonari kutoka Tanzania / misjonarz z Tanzanii /
